Friday, April 20, 2012

Penye Nia

Habari ya leo ndugu zangu katika afya njema. Leo nimerudi tena baada ya kimya kirefu (msinichoke!). Leo nataka kuzungumzia kuhusu mdogo wangu Rukia Goronga. Kwa kweli nimefurahishwa na amenifanya nijivunie kwa nia yake ya kupoteza uzito. Aliamua kuufanyia kazi uzito wake na kweli amefanikiwa. Alikua ana uzito wa kutishia afya yake, uzito wa 93kg sio uzito wa kuwa na mtu anayetaka afya njema. Lakini leo najivunia kusema mdogo wangu ameweza kupunguza kilo zaidi ya 20!Ndio, umesoma vizui, kg 20! kwa sasa ana 71.6kg kwa kweli anahitaji pongezi nyingi. Sasa hivi anajisika ana nguvu zaidi, kazini anaenda kwa kishindo chote, amebadilisha nguo zote sababu hakuweza kuvaa nguo za zamani tena. Ni hela ambayo anafurahi kuitumia kwa kununua nguo saizi ndogo kwa sababu anapendeza zaidi ya nguo zake za zamani. Way to go lil sis!

Hii inaonyesha kwamba tukitaka kitu kwa moyo wetu wote tutafanya tu, na tukiwa na watu ambao wanatusaidia kimawazo basi tutafika tunapotaka.

Nawaomba ndugu zangu, mkitaka kufanya kitu mnaweza ni kujiwekea malemgo na sababu ya kufany hicho kitu! Wengine wanaamua kuacha kunywa pombe sababu ya watoto, wengine sababu ya dini, wengine sababu ya kazi na wengine sababu ya afya zao. Sasa wewe unaamua kupunguza uzito kwa sababu gani? Sababu kubwa na ya umuhimu ni kwa ajili ya afya yako! Itunze hiyo afya yako, utunze huo mwili wako manake unao mmoja tu! I am challenging you to take action and take care of your health, you will love yourself more after this!

Wenu katika afya!
Farida

Friday, July 22, 2011

Watoto

Siku hizi watoto wetu wana "access" na vyakula vingi ambavyo sisi zamani tulikua tunaona kama ni luxury. Yogurt, Juice, Ice cream, sweets, biscuits na vingine vingi tu. Na sisi wazazi tunaona tusiwakatili raha yao na kuwapa hivyo vitu. Je, tunaangalia kiasi ambacho watoto wanakula hivyo vitu? Ukiangalia zaidi watoto wa siku hizi hawachezi kama tulivyocheza zamani. Kwanza mitaa siku hizi ina watu wengi na sio salama kwa hiyo hutaki kumruhusu mwanao akacheze mtaani, naelewa. Pili kuna michezo ya ndani ambayo pia sisi hatukuwa nayo, playstation, xbox, internet games, zote hizo zinawafanya watoto wasiwe na activities nje, wanakua na sedentary life.

Child Obesity ni shida siku hizi, watoto ma-obese wanazidi duniani. Unakuta watoto wana uzito wa mtu mzima na sisi wazazi tunajivunia kuwa na mtoto mnene, inaonyesha ni jinsi gani tunamlisha mtoto. Tunasahau kwamba watoto pia wanapata matatizo ambayo watu wazima wanapata wakiwa na uzito usiohitajika. Kuna kisukari cha watoto, watoto kutaniwa na wenziwe kwa unene walionao na hii inawashushia self esteem, n.k

Kwa hiyo mama na baba, tuwaangalie watoto wetu inapokuja suala la chakula, tuwape chakula kinachofaa na sio "junk food" zilizopo siku hizi. Tutakuwa tunawapenda zaidi kwa kuwapa hivyo vyakula kuliko kuwapa vyakula visivyofaa. Tuwahamasishe wacheze michezo ambayo itawafanya wawe active. Waruke kamba, waendeshe baisikeli, wakimbie n.k. Tukipata muda tucheze nao nje, itawasaidia wao na sisi pia. Kuna michezo mingi ambayo wazazi wanaweza kucheza na watoto, badminton, kuruka kamba, soccer au hata kufanya mashindano ya kukimbia hapo nyumbani. Itawapa mazoezi wote na pia muda wa ku-bond na mtoto. Kwa wale wanaokaa sehemu yenye bahari au ziwa, mnaweza kucheza michezo ya beach. Its fun and healthy!

Stay healthy

Thursday, June 9, 2011

KULA VIZURI LEO KWA AJILI YA BAADAE

Natumai wote hamjambo kwa siku ya leo. Nimekua kimya tena na kama kawaida yetu lazima kuna sababu! "Naandika research yangu", "kazi zimekua nyingi" n.k. Ni kweli kwamba muda unakua mdogo kwa sababu ya mambo mengi ninayofanya lakini kama nikitaka kutafuta muda wa kufanya kitu nitaupata. Na leo nimeamua kupata muda na kuandika kitu kifupi tu.

Leo nataka kuzungumzia kuhusu kujiandaa sasa hivi kwa ajili ya uzee. Watu wengi huwa tunajiandaa kipesa kwa ajili ya maisha ya baadae. Lakini wachache sana tunakua tunajiandaa kiafya kwa ajili ya maisha ya uzeeni. Tunajua wote kwamba magonjwa mengi yanakua kwa wazee, blood pressure, kisukari, mzunguko mbaya wa damu n.k. Kitu ambacho huwa tunasahau wote ni kwamba hayo magonjwa tumekua "tunayaandaa" tangu tuko vijana kwa chakula tunachokula na lifestyle tunayofuata. Chakula tunachokula kama sio kizuri kwa miili yetu kinakua kinasababisha hali ya ugonjwa ambayo itakuja kujitokeza huko mbeleni.

Kwa hiyo basi, tuangalieni vyakula tunavyokula, tuchemshe badala ya kukaanga. Tutumie mafuta mazuri (olive oil, canola oil n.k). Tule samaki kwa wingi na kupunguza 'red meat". Na pia tusisahau kufanya mazoezi. hayo ni baadhi tu ya mambo machache tunayoweza kufanya kusudi tuwe na afya nzuri.

Nawatakieni afya njema

Farida

Friday, April 29, 2011

Muda

Ni muda mrefu sasa tangu nimetuma post katika hii blog. Sijivunii na kitendo hiki. Kama watu wote tusemavyo "muda sina kabisa siku hizi", mara tunasema "nitaanza kesho", "nitakapomaliza project hii nitaanza", n.k n.k. Muda hatuupati kama hatujitahidi. Kila siku tunakua tuna kitu tunafanya, na itakua hivyo hivyo mpaka mwisho wa maisha yetu. Leo nilikua naongea na mama mmoja ambaye anataka kupunguza uzito. Kaenda kumuona dietician (kalipa hela nyingi tu) lakini hakuchukua karatasi aliyopewa kwa ajili ya kuanza program. Nilivyokua naongea nae sikuona kama ana nia ya kupunguza uzito, niliona anataka kufanya hivyo kwa sababu anajua inabidi afanye hivyo lakini hajui kama ataweza kufanya hii programm.

Sasa basi, watu wengi ambao wanataka kupunguza uzito wanakua na nia ya kupunguza uzito lakini hawana "nguvu" au imani kwamba uzito utapungua. Hii ni kwa sababu wamejaribu "njia nyingi" ikiwa ni pamoja na kujishindisha njaa ili kupunguza uzito. Kwa hiyo wanaamua kusema kwamba hawataweza. Mpaka kuwa na "turning point", labda ugonjwa au kitu kingine. Lakini utakuta mpaka muda huo ufike inakua ni vigumu zaidi kufuata afya nzuri.

Nakumbuka mume wangu kabla hajaanza program alitaka kununua saizi kubwa ya nguo sababu alizokua nazo zilikua zimeanza kumbana. Alishindwa kumbeba binti yetu vizuri sababu tumbo lilikua linamsubua na siku hiyo ndio tukaamua kwamba anaanza program!, hiyo ndio ilikua "turning point" yake. Manake tukaona sasa tutanunua nguo kubwa mpaka lini? Wiki iliyofuata akaanza kufuata "helathy lifestyle" rasmi. Na baada ya miezi minne alikua ameshafikia kwenye uzito unaofaa, na ni mwaka sasa yuko katika uzito huo huo.

Kwa hiyo ndugu zanguni tutafute "turning point" yetu wakati bado tunaweza kusudi tuweze kuanza kuangalia uzito wetu. "Turning point" yetu inabidi tuipate wakati bado tunaweza, sio kwa sababu tunaumwa sababu wakati huo unaweza kushindwa kufuata hii "lifestyle" kwa sababu ya ugonjwa.

"Turning point" zetu ziko nyingi kama tukizitafuta. Miguu kuuma, uzito wa mwili kwa ujumla, mama ana blood pressure kubwa, baba wa jirani kafariki ghafla kwa stroke, n.k, n.k. Hizi zote ni hali ambazo ukifuata "lifestyle" nzuri ya kula utaepuka matatizo haya.

Tuanze kuangalia afya zetu wakati bado tunaweza, huko mbele inakua vigumu zaidi na inakua "expensive" zaid sababu inaunganisha matibabu na kila kitu.

Nawatakieni afya njema

Wednesday, September 8, 2010

Uzito mzuri kwa afya nzuri

Kwa mama wa kiafrika mwenye mtoto wa watoto, unene ni kitu ambacho kinakubalika na kinachukuliwa kama ni maisha mazuri. Kila wakati utasikia mtu anasema "nimemuona fulani kanenepa kapendeza!" Unene umekua ukihusishwa na "mafanikio" ya maisha. Lakini siku hizi watu wengi wameona kwamba unene "sio dili" tena, ni mzuri kama bado uko kijana, active na nguvu zako. Japo unakua unaipa miguu uzito mkubwa wa kubeba mwili mnene, unakua hausikii sana sababu bado una nguvu zako. Sasa basi ikifika wakati miguu inachoka kubeba mwili mkubwa, moyo unakua umezungukwa na mafuta, mishipa inakua ina mafuta na mzunguko wa damu unakua wa shida, ndio hapo unaona tunaanza kuwatatata "maspecialist" kwa ajili ya magonjwa mbalimbali, hypertension, high cholestrol, kisukari, magonjwa ya moyo to name few.
Sasa ndugu zangu, ni wakati ambao inabidi tuangalie miili yetu kwa ajili ya watoto wetu, waume zetu na hasa hasa kwa ajili yetu wenyewe. Wakati ule wa kusema "unene dili" umepita na tujiangalie miili yetu, weather tuna watoto au hatuna, uzito wetu tunaweza kuungalia na kuuweka katika "uzito mzuri", kama blog hii inavyosema.
Nawatakia afya njema

Monday, August 30, 2010

Njia mbalimbali za kupunguza uzito





images courtesy of fitnessmag

Mazoezi na vyakula ni muhimu katika kupunguza na ku-mantain uzito mzuri. Katika post zijazo nitakuwa naelezea aina za mazoezi na vyakula. Pia napokea ideas kama kuna kit utapenda nizungumzie nitumie email.

Friday, June 25, 2010

Why do some weight loss programs succeed?

While there is no “one size fits all” solution to lifelong, healthy weight loss, try these tips:

  • Lifestyle change – Permanent weight loss is not something that a “quick-fix” diet can achieve. Instead, think about weight loss as a permanent lifestyle change. You are making a commitment to your health for life. Various popular diets can help to jump-start your weight loss, but permanent changes in your lifestyle and food choices are what will work long term.
  • Find a cheering section – Social support means a lot. Our planned program to come will use group support to impact weight loss and lifelong healthy eating. Seek out support, whether in the form of family, friends, or a support group, so that you can get the encouragement you need.
  • Commit to a plan and stick to it – Experiment until you find a good, long-term plan that helps you lose the weight and maintain that loss in a way that works for you. If you cut out just 100 calories a day you could lose 10 pounds in a year. Remember, one 330ml can of soda can contain 150 calories.
  • Lose weight slowly. Losing weight too fast can take a toll on your nervous system, making you feel sluggish, drained, and sick. When you drop a lot of weight quickly, you’re actually losing mostly water and muscle rather than fat. Aim to lose 0.5 to 1.5 kg a week to ensure healthy weight loss.
  • Stay motivated and keep track – Short-term goals, like wanting to fit into a wedding gown, usually don’t work as well as goals like wanting to feel more confident or become healthier for your children’s sakes. Keep a food journal or weigh yourself regularly. Find and use tools that help keep you motivated. Stay focused: when frustration and temptation strike, concentrate on the many benefits you will reap from being healthier and leaner.
Stay healthy